lundi 2 septembre 2013

ELLE S'EN EST ALLEE: QUI EST Sr. LOUISE DE LA MISERICORDE?


1.    IDENTITE
Kwa majina, dada yetu alikuwa anaitwa : KAVIRA  MWENDAPOLE Louise
Baba yake ni : KAMBALE KINAVA  Donat; Na Mama yake ni : KASWERA KATSUVA MUGHUMBIRWA Victorine, wote wako hai.
Dada  yetu alizaliwa pa Mangango, tarehe ine mwezi wa tatu  mwaka elfu moja mia kenda  sabini na saba Le 04/03/ 1977.
2.    Maisha ya kikristu
Dada Mwendapole alibatizwa pa Makeke- Mangina,  tarehe ine mwezi wa ine  mwaka elfu moja mia kenda sabini na saba Le 04/04/1977, akapewa jina la Louise.
Alipokea Komunyo ya kwanza pa Beni Tamende, tarehe kumi na mbili  mwezi wa tano  mwaka elfu moja mia kenda makumi munane na nane.Le 12/05/1988
Alipokea sacramenti ya usabitisho pa Bingo, tarehe kumi na saba  mwezi wa saba  mwaka elfu moja mia kenda   tisini na moja Le 17/07/1991.
3.    MASOMO YAKE
Masomo ya msingi: pa Bundji  tangu   mwaka elfu moja mia kenda makumi mnane  na tano 1985 mpaka  mwaka  elfu moja mia kenda makumi mnane na kenda 1989, akaendelea pale Bingo tangu   mwaka elfu moja mia kenda makumi mnane  na kenda 1989 mpaka mwaka elfu moja mia kenda tisini na moja  1991.
Masomo ya kisekondari, pa Bingo tangu  mwaka elfu moja mia kenda tisini na mmoja 1991, mpaka  mwaka elfu moja mia kenda tisini  na tano 1995,akendelea pa Katwa tangu  mwaka elfu moja mia kenda tisini na tano 1995 mpaka mwaka elfu moja mia kenda  tisini na kenda 1999. Hapo akapewa diplome d’Etat en Pédagogie Générale.
                       
4.    MAISHA YA KITAWA
Formation: Dada Kavira Mwendapole, alikusudia kujitolea kwa Mungu katika shirika ya mabikira Oblates de l’Assomption. Akapokelewa kama postulante tarehe makumi mawili na tano  mwezi wa saba  mwaka elfu mbili  na moja Le 25/07/2001 pa Mapendano, postulat Marie Correnson; Baada ya myaka miwili, akaanza noviciati tarehe kumi na tatu  mwezi wa nane mwaka elfu mbili  na tatu Le 13/08/2003 au noviciat Notre Dame de l’Espérance.
Dada Louise akaweka  nadhiri zake za kwanza tarehe kumi na mbili  mwezi wa nane  mwaka elfu mbili   na tano Le 12/08/2005. Akapokea jina la Soeur Louise de la miséricorde .
 Akaweka nadhiri za maisha  tarehe kumi  na mbili  mwezi wa nane  mwaka elfu mbili  kumi na mbili  Le  12/08/2012.
5.    MAISHA YA KITUME
Tangu  mwaka elfu mbili   na mmoja 2001 mpka mwaka elfu mbili   na tatu 2003, alikuwa mwalimu pa ecole maternelle Mapendano.
Tangu   mwaka elfu mbili na tano  2005 mpaka mwaka elfu mbili   na sita 2006, akatumika pa Centre Hospitalier ya Wanamahika kama perceptrice, baada ya mwaka mmoja, akatumwa kama misionari inchini  Tanzania, pale Arusha, hapo alitumika kama katibu kwa Baba Arkiaskofu muda wa miaka mitano yaani tangu   mwaka elfu mbili   na sita 2006, mpaka  mwaka elfu mbili  kumi  na mmoja 2011. Na ndipo aliomba  probation yake ili ajitayarishe vizuri kwa nadhiri ya milele, jinsi ilivyo kanuni ya shirika letu. atatumwa Musienene ili afuate mafunzo yanayofaa pamoja na wenzake.
6.    FAZILA ZAKE
Sœur Louise, alikuwa na imani sabiti Kwa Mungu, imani yake ilionekana wakati wa majaribu na ugonjwa.  Yeye mwenyewe aliomba mapadre waje kila mara kumsomea misa, na kumsikiliza (accompagnement spirituel et sacrements), hata juzi amepokea sacrementi ya upatanisho na ya upako wa wagonjwa.
 Wote waliofika kumuona, walimkuta na kicheko midomoni, na japo maumivu makali, alizungumuza na wageni na moyo wa matumaini.
Alikuwa mpole kweli, hakuwa na matata na wenzake, alikuwa  mkarimu sana, mwenye juhudi kwa kuwatumikia, na kuwatendea mema watu wengi bila ubaguzi wowote.
7.    UGONJWA  NA KIFO CHAKE
Sœur Louise alianzagonjwa kwa mwezi wa kumi na mmoja, wa mwaka jana, yaani 2012, akapewa matibabu pa C H Wanamahika, alipopata nafuu, akaendelea na masomo yake pale UCG, baada ya mwezi mmoja, afia yake akadhoofika ; akapelekwa Musiennene ili atunzwe vema zaidi. Waganga wajitahidi kumpa  dawa zinazofaa kwa ugonjwa wake, alakini hakupona. Ndipo, kwa mwezi wa pili wa mwaka huu, akapelekwa Kampala ili apate kutunzwa vema zaidi, pale pia waganga wakamshurulikia kwa namna yote, alakini dada yetu hakupata nafuu . Baada ya miezi miwili, akarudi hapa DRC ; akabaki nyumbani mwetu pa école des filles  akishurulikiwa na mabikira wenzake, akipata dawa  za kila aina, alakini afia yake ikawa mbovu zaidi na zaidi. Watu wengi, wajamaa, mapadre na watawa walifika pale kumsalimia kila siku . ameaga dunia leo tarehe mosi mwezi wa kenda mwaka elfu mbili na kumi na tatu , na saa kumi na mbili na dakika makumi mawili . Le 1 / 09/ 2013 à 6H20.
 SHUKRANI
§  Shukrani zetu zimuendee Mungu mwenyezi, aliye chemchem ya uzima, ametupa tena ametwaa, Jina lake lipewe sifa.
§  Shukrani zimuendee Mhashamu Baba Askofu aliyekubali kusimamia ibada hii takatifu ya kumuombea Sœur Louise.
§  Twawashukuru ma Padre na watawa wote waliofika kusali pamoja nasi.
§  Twawashukuru pia nyinyi wote muliokubali kuacha kazi zenu na kuja kutufariji. Mungu awabariki ninyi nyote.
§  Baada misa hii, tutapeleka dada wetu kwa makao yake ya mwisho pale Musienene. Baada ya maziko, tutabaki uwanjani mwa nyumba yetu, communauté saint rosaire, ili kugawa maji kidogo iliyoandaliwa kwa siku ya leo.

3 commentaires:

  1. Oups ! Chère Louise, nous nous confions à ta prière auprès du Père. Repose en paix. Mais l'émotion est grande...

    RépondreSupprimer